Friday, November 30, 2012

UKUAJI WA UCHUMI NCHINI HAUTAWASADIA WATANZANIA-WADAU




UKUAJI wa uchumi nchini hautawasaidia  watanzania kutoka kwenye lindi la umaskini iwapo njia mbadala  hazitachukuliwa kudhibiti rushwa na  uhusiano usiosawia  baina ya serikali na sekta binafsi, imeelezwa.

Wakichangia mada kuhusu wajibu  wa sekta binafsi katika kupunguza umaskini Jijini Dar es salaam juzi, wadau mbalimbali wa maendeleo walisema kuwa jitahada za Tanzania kukuza uchumi wake hazitakuwa na msaada wowote kwa Watanzania katika kupunguza umaskini iwapo rushwa na  uhusiano hasi baina ya Serikali na sekta binafsi havitaondolewa.

Walisema kuwa uhusiano uliopo baina ya Serikali na sekta binafsi hauna usawa kwani sekta binafsi imekuwa na nguvu nyingi kuliko Serikali na kusababisha malengo na jitaha za  Serikali kupunguza umaskini nchini kutofikiwa ipasavyo.

Mwendesha Walsha ya kujadili wajibu wa Sekta binafsi katika jitahada za kupunguza umaskini Bakari Bujari (kushoto0 akiwa na Mkurugenzi Msaidizi wa British Council Dkt Conor Snowden wakati wa uzinduzi wa Walsha hiyo Jijini Dar es salaam juzi.
Akizungumza katika mdahalo huo Afisa Mtendaji wa Taasisi ya kimataifa  isiyo ya Kiserikali ya  VSO  Marg Mayne alisema kuwa taarifa ya Benki ya Dunia inaonyesha Uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi lakini ukuaji huo umeshindwa kuwakomboa Watanzania wengi hususani waishio vijijini kutoka kwenye lindi la umaskini bali umeongeza tofauti kati ya maskini na matajiri.

Aliongeza kuwa ugunduzi wa gesi na mafuta nchini unaotarajia kukuza uchumi wa nchi kwa aslimia 6.5 hadi 7 hautaleta mabadiliko yoyote iwapo mfumo wa sasa wa uhusiano baina ya serikali na sekta binafsi hautavunjwa.
Alishauri uanzishwaji wa ushirikiano wa kina na ushawishi uliosawa baina ya wadau wa maendeleo na sekta binafsi ambao utaenda mbele zaidi ya sera ya Wajibu wa kampuni kwa jamii (CSR) ili kuongeza mchango mkubwa wa makampuni katika jitahada za kupambana na kupunguza umaskini nchini.

Rananie Kunanayagam, Mkuu wa Utendaji wa Jamii Kampuni ya BG group alisema ushirikiano wa Serikali na sekta binafsi si jambo jipya duniani kwani lilishakuwepo miaka 15 hadi 20 iliyopita katika nchi nyingi zinazoendelea ikiwemo Tanzania lakini umaskini bado upo palepale hivyo anahitajika mtu wa kusimamia uhusianobaina  ya Serikali na sekta binafsi.
“Kunahitajika uwepo wa mtu au taasisi katikati ya Serikali na Sekta binafsi ambaye hatang’ata upande wowote na kuwashawishi wote kutekeleza majukumu yao kwa usahihi” alibainisha Kunanayagam.

Mshiriki wa mdahalo wa kujadili wajibu wa Sekta binafsi katika jitahada za kupunguza umaskini nchini akitoa maoni juu ya mada hiyo juzi katika ukumbi wa British Council.Jijini Dar es salaam juzi.
Naye Mkurugenzi Mkazi wa UNDP nchini Phillipe Poinsot alisema kuwa lazima kuwe na mgawanyo sawa wa wajibu baina ya Serikali na sekta binafsi katika kupambana na umaskini na pia Serikali izidishe uhusiano ndani ya Sekta binafsi.

Alisema kuwa Serikali ihakikishe inatengeneza miundombinu na mazingira rafiki kwa sekta binafsi kwa kutengeneza barabara safi, umeme wa uhakika, sheria thabiti, usimamizi mzuri wa rasilimali,  wasomi na viongozi  makini wasiopenda rushwa wakati huohuo  sekta binafsi ina wajibu wa kutoa kodi halali, uwazi katika uendeshaji, kuendeleza teknolojia na kutoa ajira stahiki kwa Watanzania.

Mjumbe wa Mdahalo huo Semkai Kilonzo alisema uwepo wa miongozo mingi inayohusika na jitahada za kupunguza na kupambana na umaskini kama MKUKUTA, Dira ya 2025, Kilimo Kwanza na mingine ni chanzo kikubwa cha ukuaji wa uchumi nchini kushindwa kuwakomboa Watanzania kutoka kwenye lindi la umaskini.
“Uwepo wa Miongozo mingi kwa wakati mmoja  kama MKUKUTA, Mkurabita, Kilimo Kwanza kunachanganya Wadau wa maendeleo na pia imekuwa haina ushirikishwaji wa Wananchi katika kufanya maamuzi ya maendeleo yao hivyo inashindwa kupata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa wadau” alisema Kilonzo.

Mdahalo huo Uliandaliwa na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya VSO International ikishirikana na BG Tanzania na British Council ambapo wadau walitaka rushwa itokomezwe,  uwazi wa utendaji katika makampuni na serikali, kuanzishwa kwa sera na sheria inayotoa kiwango na aina za miradi inayoweza kufanywa na makampuni katika Sera ya Wajibu wa Kampuni kwa Jamii (CSR).




Tuesday, November 27, 2012

FASTJET YAZINDUA RASMI SAFARI ZA NDEGE MIKOANI



KAMPUNI ya ndege ya Fastjet  imezindua rasmi safari zake nchini katika Mikoa mitatu ya Dar es salaam, Mwanza na Kilimanjaro kwa safari mbili za kila siku Dar-Mwanza na Dar-Kilimanjaro na ndege aina ya Airbus A319.  

Afisa Mtendaji wa Fastjet Ed Winter kushoto akiwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi Charles Tizeba wakati wa uzinduzi wa safari ndege za kampuni hiyo.
Akizungumza katika Uzinduzi huo leo Jijini Dar es salaam mgeni rasmi Naibu Waziri wa Uchukuzi Charles Tizeba alisema kuwa kuanza kwa safari za ndege za kampuni hiyo inayotoa huduma hiyo kwa bei rahisi kutachangia ukuajiw auchumi kwa kasi sana kwa kuongeza idadi ya Watalii, kutaongeza mzunguko wa biashara na pia kurahisisha safari binafsi za Watanzania.

Tizeba alisema kuwa Serikali inawaunga mkono sekta binafsi hususani katika usafirishaji wa naga kwa kurekebisha Viwanja vilivyopo na kuendelea kuvitengeneza vipya kikiewemo cha Songwe Mbeya kinachotarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi desemba Mwaka huu. Aliongeza kuwa kwa sasa wanarekebisha Viwanja Vya Tabora, Kigoma na Mafia huku Kiwanja ch mpada kikiwa kimezinduliwa hivi karibuni.

 Hata hivyo aliitaka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini(TAA) kuhakiksha inarekebisha miundombinu na huduma za Viwanja vya Mwanza na Kilimanjaro ili kukidhi ongezeko la mahitaji ya wasafiri watakaotumia Viwanja hivyo.

 Afisa Mtendaji wa Kampuni hiyo Edward Winter alisema kuwa Kampuni yake ina uzoefu mkubwa kufanya biashara hiyo kwa bei nafuu hivyo watanzania wasihofie kushindwa kuendelea kwa kampuni hiyo na kuongez kuwa Safari nyingi zaidi zitaongezwa katika nchi nne za afrika za Kenya, Ghana, Rwanda na Angola.

 Aliongeza kuwa huduma zinazotolewa katika ndege hiyo ni za kisasa na zinazokidhi viwango vya Kimataifa vikiwemo viwango vya Ulaya (European Airline Standards). Hivyo basi Watanzania wachacharikie huduma hiyo ya haraka na bei rahisi kutokea nchini.

Naibu Waziri wa Uchukuzi Charles Tizeba akitoa hotuba wakati wa uzinduzi wa safari za ndege za Fastjet.

Afisa Mtendaji wa Fastjet Ed Winter akihutubia wadau wakati wa uzinduzi wa safari za  ndege za Kampuni hiyo.

Airbus A319 ya Kampuni ya Fastjet katika picha kabla ya safari ya Uzinduzi mapema leo asubuhi

Maofisa wa Fastjet wakijadilaiana kabla ya ndege Airbus A319 kufanya safari ya Uzinduzi Jijini Dar es salaam

Waandishi wa Habari wakipata maelezo kuhusu safari za ndege za Kampuni ya Fastjet.


Naibu Waziri wa Uchukuzi Charles Tizeba kushoto akipewa maelekezo  juu ya ndege ya Airbus A319

Wahudumu wa Fastjet wakiwa katika pozi wakati wa uzinduzi huo.
Safari za ndege hizo zinatarajiwa kuanza mapema keshokutwa Alhamisi ya tarehe 29 katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam na gharma yake kuwa ya chini sana ya sh 32000 kwa sfari moja bila kodi sawa na dola 20 za Kimarekani. Hata hivyo gharama za safari hizo zinabadilika pindi muda wa kusafiri unapokaribia.
Hivi ni baadhi ya vitafunwa vinavyopatikana ndani ya ndege ya Fastjet Airbus A319

Watanzania wamehimizwa kuwahi kukata tiketi ili kupata huduma hiyo kwa bei nafuu sana kwani kuchelewa kukata tiketi kutaongeza kiwango cha nauli.

R.I.P SHARO MILIONEA

Nuzulack Dausen

Kifo cha Msanii wa Maigizo na Muziki Hussein Mkiety a.k.a Sharo Milionea kimenishtua sana. Nilipoipata habari ya kifo chake mapema leo asubuhi nilidhani rafiki zangu wananitania kwa kuwa msanii huyu alikuwa ni  maarufu wa vituko na vichekesho vingi na alishika akili za watanzania wengi kwa staili yake ya Kisharobaro hivyo walitaka tu kunighiribu akili yangu. 


Hata hivyo haukupita muda mrefu taarifa zikawa zimeshasambaa kwenye vituo mbalimbali vya habari na kufanya taarifa hiyo kuwa rasmi. Taarifa hizo zinathibitisha kifo chake kilichosababishwa na ajali ya gari gari yenye namba T478 BVR Toyota Harrier alilokuwa akiliendesha katika kijiji cha Lusanga Wilayani Muheza Mkoani Tanga na kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa  Tanga, Constatine Masawe alithibitisha kutokea.  

Binafsi nautambua mchango wa Sharo Milionea katika gemu la Bongo Movies na Bongo Fleva. Uwepo wa Sharo Milionea katika gemu kwa muda mfupi kuliamsha ari ya wasanii wengi wachanga kuingia kwenye gemu na hata wale wakubwa kukaza ili kukabilana na ushindani mkubwa alokuwa ameuanzisha Sharo Milionea.

Kwa muda huo mfupi katika muziki na filamu Sharo amekuwa gumzo miongoni mwa wadau wa muziki na filamu kwa staili zake ambazo zimekua zikitoa burudani safi ya tofauti na wasanii wengine.

“Umebugi meeni” “nasubiri mrija meeni” ni baadhi tu ya maneno ya Sharo yaliyozoeleka midomoni mwa mashabiki wake. Maneno hayo hayakumpa tu umaarufu yemwenyewe bali mpaka baadhi ya bendi za Dansi ziliyatumia. Watoto mitaani na baadhi ya watu wazima walitumia maneno hayo kutaniana.

Binafsi nimesikitishwa sana na kifo chake lakini hatuna cha kufanya kwa kuwa yote hayo ni mipango ya Mungu. Yeye ametangulia, sisi tutafuatia.

Nawapa pole ndugu wa karibu wa marehemu Sharo Milionea, Wasanii wote wa Bongo Movies na Bongo Fleva, Mashabiki na Watanzania wote kwa ujumla kwa kuondokewa na Msanii muhimu sana katika maendeleo ya sanaa nchini.

Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe. Mungu amlaze mahali pema peponi Sharo Milionea.








Monday, November 26, 2012

WAZIRI WA ULINZI WA ISRAEL ATANGAZA KUJIUZURU




Jerusalem 
Waziri wa Ulinzi wa Irael Barak Ehud akitangaza kujiuzuru kwenye siasa mapema leo hii Jijini Tel Aviv. Picha na AFP

Waziri wa Ulinzi wa Israel Ehud Barak ametangaza kujiuzulu rasmi kwenye Siasa  mapema leo hii Jijini Tel Aviv. Amesema kuwa kujiudhuru huko kutaanza mapema  mwezi Januari mwakani  ili aweze kupata muda mwingi wa kukaa na Familia yake. 

Kujiudhuru kwake kunakufuatia kipindi kigumu kwa Israel ambayo inashuhudia mapigano makali dhidi kundi la Wanangamgambo wa Hamas ambapo siku nane za mapigano wameshauawa watu zaidi ya 160 wengi wao wakiwa ni Wapalestina wa ukanda wa Gaza.

Barak kajiudhuru baada ya kazi ndefu ya Siasa aliyoifanya nchini humo na aliongeza kuwa hata shiriki Uchaguzi ujao utakaofanyika mapema mwezi Januari..




Friday, November 23, 2012

SKOL BUILDING CONTRACTORS YATOA AJIRA MPYA



SKOL BUILDING CONTRACTORS LTD.
P. O. BOX 7963 ~ LINDI/LIVINGSTONE ST. ~ DAR ES SALAAM ~ TANZANIA
Phone 2774065, 2774064 ~ Fax 2774052 ~ Mobile Phone 0773298888, 0712 797963 ~ Email vincent@skol.co.tz
Website: www.skol.co.tz
VACANCIES
Skol Building Contractors Company is the Civil Engineering Contractor registered with the Contractors Registration Board under Class One. We have expertise in Civil and Building including production of precast building materials.
Skol Building Contractors Company Limited wishes to recruit qualified, energetic and committed candidates to fill the following positions:

     JOB POSITION: HUMAN RESOURCES & ADMINISTRATION OFFICER
POSITION TITLE
 HR & ADMINISTRATION OFFICER

ORGANIZATIONALRELATIONSHIPS
Ø  Works in the HR & Administration department reporting directly to the Director of Human Resources and Administration.
      Supervises operative staff; Office Attendants, Security Guards, Front Office Executive etc.
KEY DUTIES AND RESPONSIBILITIES
      Provide assistance in all HR- management aspects; recruitment, training & development, labor relations occupational    safety/health, planning, job evaluation etc. 

      Responsible for administration works, insurance matters , budget , staff transport service ,staff medical treatment and service , office accommodation ,etc
      Responsible for payment of utility service (water, electricity ,telephone services)
      Ensures security service to the company’s properties
      Undertakes /supervises secretarial services
       Handling of company’s incoming  and outgoing mails /document
      Responsible for office stationeries , general cleanliness of office premises ,kitchen /canteen
      Deals with general disciplinary matters of his /her subordinates
     Conducts performance Review of his / her subordinate
      Secretary to the Management committee meetings workers meeting etc.
      Performs human resources activities as assigned by his/her supervisor
   
QUALIFICATIONS AND EXPERIENCE
      Holder of a diploma/ degree in HR / Public Administration
      Working experience of 2-3 years as administration officer
      Well versed with labor relations Act 2004 and Code of Good Practice 2007


JOB TITLE
SAFETY,HEALTH & ENVIRONMENTAL OFFICER
ORGANISATIONAL RELATIONSHIP
      Works in the  HR & Administration Department Reporting of  Human Resources & Administration  
      Supervises all safe, Health & Environmental STAFF

·         Develop controls for identified   hazards. Coordinate the implementation of controls from results of hazards analysis .Measure and evaluate the effectiveness of the hazard control system, policies and procedures and recommend changes that reflect improved opportunities to eliminate   workplace   accidents and injuries.
·         Direct or assist in the development of specialized education and training materials. Conduct specialized safety and environmental training programs to communicate hazard control information .Assist in new employee occupational health, safety and environmental orientation.
·         Conduct Safety Committee meetings.
·         Compile, analyze, interpret and report and report accident, loss and exposure statistical data; prepare comprehensive recommendations for corrective action to eliminate or minimize potential hazards .Review injury and property damage reports. Responsible for the overall administration worker’s compensation program.
·         Direct environmental compliance programs related to hazardous wastes, air permitting, water pollution control, and community right-to-know programs.
·         Incorporate essential occupational health, safety, and environmental requirements in all purchasing and control actions .Recommend the purchases of safety equipment and supplies.
·         Facilitate the registrations of new projects, Annual statutory inspections and medical examinations conducted by SKOL.
·         Carrying out fire drills.
·         Perform other related duties as directed that correspond to the overall function of this position.
EDUCATIONAL
QUALIFICATIONS
AND WORKING EXPERIENCE
·         Bachelor’s degree or Advance Diploma in Environmental Science, Engineering, Industrial Engineering, with training in Safety and Health issues (NOSH), or a related field is preferred.
·         Minimum 3-5 years of experience within the Environmental Health and Safety function required.
·         Proven leadership and team work skills with demonstration.
TRAINING










Must have knowledge or training in the following:
·         Occupation health, safety and environmental   compliance with applicable government (OSHA) regulations and standards.
·         Demonstrated knowledge of delivering hands on health, and environmental training
·         Ability to develop, implements, and coordinate comprehensive health and safety accident prevention programs.

SKILLS
·         Strong communication skills, both verbal and written (training/ presentations/ report whiting )
·         Ability to lead and direct teams and / or committees
·         Strong Computer skills in Microsoft Office (Word, Excel and PowerPoint
·         Skilled in the standards, practices and procedures within the health safety and environmental fields.
·          Ability to work all levels within and organization and ability to work in a diverse workgroup
·         Demonstrated strong interpersonal skills


JOB POSITION: PERSONAL SECRETARY- CEO

POSITION TITLE
PERSONAL SECRETARY -CEO

ORGANIZATIONAL RELATIONSHIPS
       Works in the CEO’s office.
     Supervises CEO’s operative staff.
KEY DUTIES AND RESPONSIBILITIES
     Typing printing of document , reports etc,
      Photocopying scanning faxing documents
      Files documents in relevant files in CEO office
      Receives and directs visitors to relevant offices
      Servicing committee meetings
      Takes proper care of all machines under her charge and ensure they are used for official work only.
      Attends telephone calls and takes message for respective officer
      Make sure there are all necessary facilities for proper job performance
     Makes travel arrangements for CEO and senior officers.
      Receives and scrutinizes incoming mails
      Provides secretarial services to senior officers
     Keeps record of events in the CEO office
     Handles personal and confidential matters in the CEO’S office
      Communicates and answers inquiries and provides information to visitors and other customers.
      Keeps office in well arranged and tidy appearance.
      Distribution of general correspondences incoming /outgoing mails
      Keeps and schedules CEO’S appointments
      Ensures that CEO’S office operates at a high level of efficiency.

QUALIFICATION AND EXPERIENCE


     Holder of Diploma in Secretarial studies from a recognized institute like Tanzania Public Service college (TPSC)
     Three year of working experience as PS.
      Fluent in both Kiswahili and English languages





CAMP MANAGER.
REMUNERATION
A competitive remuneration will be offered to the successful candicates for the above positions basing on qualification and experience.

MODE OF APPLICATION
Interested candidates are invited to submit their application letters attached with a detailed ,curriculum vitae  passport size photo ncluding names and contact details of their three referees  to the address below not  latter than 18th December  2012
Chief Executive Officer
SKOL Building Contractors Company  Limited
Plot 715/46 Shekilango Road
P.O.BOX 7963
Dar es Salaam, Tanzania
Please, the title of the position applied for should be marked on top of the envelope;short of which will make the application invalid.Furthermore,if you have not heard from us with in three weeks after the closing date,kindly, assume that your application was unsuccessful.The detailed advertisement is also found in our website  www.skol.co.tz .SKOL Building  Contractors Company Limited is an equal opportunity employer.