Saturday, February 13, 2016

Wewe ndiye Valentine wangu wa kweli

Nuzulack Dausen
Twitter: @nuzulack
Kwako mke wangu mtarajiwa. Valentine imewadia tena.
Najua bado una huzuni na wasiwasi nimekutelekeza. Una hofu na miaka inavyokwenda kasi bila kunipata mimi, kipenzi chako cha kweli.
Rafiki zako ambao mwaka jana walikuwa waseja kama wewe, tayari wameshaolewa ama kuchumbiwa. Na wewe umeshiriki kikamilifu kuwaoza.
Lakini bado wanisubiri nifike, nije kukuoa licha ya kuwa miaka inazidi kuyoyoma. Hujakata tamaa.
Nafahamu bayana mabarobaro wengi hujipitisha pitisha na kukulaghai uwakubali. Lakini moyo wako u thabiti na hujawapa nafasi. Ndoto yako ya kuwa na mimi imekutawala siku zote.
Mwaka jana nilikusihi usifadhaike wakati wa sherehe za valentine. Nilikusihi usisitetereke na rafiki zako waliokuwa wakiringa kwa zawadi walizopewa na mabwana zao. Mwaka huu pia Valentine inabisha hodi.
Hujapata zawadi yoyote wala ujumbe mzuri kwenye simu yako. Ungetamani umpate mtu wa kukubembeleza ukichoka na kazi na wakati ukiumwa.
Ungetamani uwe na mfalme wa moyo wako ambaye muda wote angekuwa na wewe akikujali na kukupa mapenzi moto.
Kiufupi, unamtaka mume wa kukufanya mke mwema na chaguo la kweli. Lakini bado giza linakuzuia usione nuru. Nuru ya maisha mapya ya kuwa wawili na kutekeleza masharti ya vitabu vya dini.
Tafadhari vumilia.  Hata Valentine hii imefika na hujaniona, usifadhaike. Narudia usikate tamaa. Nipo nakuja japo sijafika karibu yako. Sidhani kama ni Valentine hii lakini utaniona.
Usitishike na rafiki zako wanaokutambishia zawadi za smartphone walizopewa na mabwana wanaotaka kuwachezea. Wala usibabaike na selfie zao wanazoweka mtandaoni wakiweka ‘status’ za “Ready for Valentine (Tayari kwa valentine).”
Mimi ndiyo zawadi yako ya kweli. Zawadi ya kudumu ya maisha yako. Duniani na mbinguni. Upendo wangu kwako ni zaidi ya zawadi ya smartphone au Vitz. Upendo wangu haubanwi na muda eti mpaka siku ya Valentine pekee la hasha. Mimi ni wako siku zote.
Nakupenda kila siku japo hatujawahi onana. Nakuw
aza wakati wote na nakupenda kutokana na uzuri wa asili ulionao, heshima, upole, werevu, ubunifu na uvumilivu wako.
Siyo mapepe wala waruwaru wa kukufanya nyumbani kwetu wakukatae. Huropoki ovyo na kulalamika mara kwa mara mbele za watu hata kama mtu kakukosea mara 1,000. Huvai nguo za vipisi zikakuonyesha maungo yako kana kwamba upo sokoni.
Huweki nyusi za bandia na kujisiliba rangi tofauti usoni ukaonekana kama kichekesho mbele za watu. Hujawahi waza kuweka makalio ya ziada kwa sababu una uhakika mimi situmii maumbo hayo kama kigezo cha mwanamke mzuri.
Hutumi mara kwa mara picha mtandaoni kuonyesha unaponda raha kwa kuwa unajua mwanamke bora hupenda kusitiri mwenendo wa maisha yake binafsi na ya nyumbani.
Hakika wewe ndiyo Valentine wangu. Na mimi ndiyo Valentine wako wa kweli. Nisubiri nije nikupoze moyo. Nivumilie kidogo tu. Nikifika, sitachelewa, nitakutolea posa na kukuoa.
Nikutakie heri ya wapendanao huko uliko japo kila siku hufanya hivyo. Nakupenda mchumba wangu.


Thursday, November 19, 2015

Uwaziri Mkuu wa Majaliwa unavyoweza kujaliwa zaidi

Baada ya Rais John Magufuli kupendekeza jina la Kassim Majaliwa kuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya awamu ya tano na hatimaye kupitishwa na Bunge, habari zinazozunguka kwa sasa nchini ni kwamba kiongozi huyo mpya ataweza jukumu hilo zito.
Uteuzi wa Majaliwa unaokena kama ni ‘surprise’ kwa Watanzania waliowengi. Ndiyo, huenda kweli ni surprise kwa sababu mwanasiasa huyo si mwingi wa kutafuta ujiko kama wengine.
Inawezekana kweli ikawa Surprise kwa kuwa wengi hawakutarajia kuwa Dk Magufuli angefanya uteuzi wakenje ya miamba ya siasa iliyozoeleka na iliyokuwa ikitajwa kama William Lukuvi na Dk Harrison Mwakyembe.
Kwa aina ya uteuzi huo wa Rais hapana shaka swali la je, Majaliwa atakitendea haki cheo hicho hasa katika Seikali inayojinasibu kwa “Hapa Kazi Tu”, haliepukiki. Na maswali mengi kama hayo yataibuka kila uchwao katika siku hizi za awali ambazo Mbunge huyo wa Ruangwa atakuwa akianza kutekeleza majukumu yake.
Kwa mtazamo wangu, Majaliwa anaweza kwenda na kasi ya Magufuli kwa asilimia 100. Si kwenda nayo yu bali hata kuituliza kasi hiyo pale itakapoonekana kuzidi na kuleta hatari.
Kama mwanahabari nafahamu utendaji wa Majaliwa kupitia nafasi zake alizopitia hasa ya Naibu Waziri wa Ofisi ya Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tamisemi (Elimu) ambayo baadhi ya mambo nilikuwa nikiyafutilia kwa karibu likiwemo agizo la rais mstaafu Jakaya Kiwkete la ujenzi wa maabara kwa kila shule ya Sekondari ya Kata.
Hivyo, matokeo ya utendaji bora wa Majaliwa yatachangiwa zaidi na baadhi ya mambo yafuatayo:-

  1. Hafahamiki sana
Licha ya kuwa alikuwa Naibu Waziri katika Serikali iliyopita, Majaliwa siyo miongoni mwa watu maarufu sana kiasi cha mfumo wake wa usimamizi na utendaji kufahamika bayana miongoni mwa watumishi wa umma na wananchi.
Pamoja na kutofahamika sana, Waziri Mkuu ni mtendaji. Ni mtendaji asiyefahamika na wengi. Wengi wanaomfahamu, angalau kasi yake, ni wale waliopo Tamisemi na kwenye sekta ya elimu. Vivyo, wanasiasa wanaoweza kujinadi kuwa wanamfahamu ni wale tu waliokuwa kwenye Kamati mbalimbali za Bunge ambazo zilikuwa zikishirikiana mara kwa mara na Tamisemi.
Sifa hizo zikijumulishwa na uchapakazi wa bosi wake, Dk Magufuli inapatikana picha ya moja kwa moja kuwa watumishi hawatakuwa na njia nyingine zaidi ya kujituma kufanya kazi kutokana na kutojua aina ya misimamo ya Majaliwa.
Matokeo hayo, yatamsaidia vyema mwalimu huyo wa zamani kuwasimamia mawaziri wake ambao bila shaka wengi watakuwa wapya kwenye Baraza la Mawaziri linalotarajiwa kuundwa hivi karibuni.

  1. Presha ya kukilinda chama tawala

Kama ilivyo kwa Rais, Majaliwa naye atakuwa na kibarua kigumu cha kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha anasaidia kuiokoa CCM kutoka madarakani miaka mitano ijayo.
Kwa maana hiyo, hataweza kuruhusu uzembe wowote ndani ya utumishi wa umma ambao huenda ukaipeleka CCM kwenye kaburi la sahau na kuiacha nchi chini ya upinzani.
Ushindani uliokuwepo katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25 ni salamu tu kwa Serikali ya JPM ambayo Waziri Mkuu hubeba mizigo kibao ya Serikali pale ufanisi unapopitia mlango wa nyuma.
Hofu hiyo, itasaidia mbunge huyo wa Ruangwa afanikiwe kuitumikia nafasi yake vyema na kuonekana ni mchapakazi na kujibu maswali yanayojitokeza kwa sasa.

  1. Kulinda kibarua chake
Hakuna ubishi kuwa baada ya kuitumikia nafasi hiyo kwa kipindi kifupi, Majaliwa atavutiwa kuendelea kuitumikia ili kibarua kisiote nyasi. Hatakubali kirahisi ibara ya 53A ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imng’oe na kuweka historia kwa mara ya kwanza nchini.
Hatothubutu hata kidogo akina Tundu Lissu au Zitto Kabwe waanzishe hoja za kuwa na imani na Waziri Mkuu wakati ana uwezo wa kuzuia hali hiyo mapema kwa kufanya kazi kwa bidii.
Hivyo, nia hiyo njema ya kupalilia kibarua moja kwa moja itamsaidia kuchapa kazi na hata kukwepa vizingiti vya kumwangusha hapo mbeleni.
Kwa vyovyote itakavyokuwa, Majaliwa kama mwanasiasa yoyote anafaa kuwa Waziri Mkuu. Lakini kikwazo kikubwa kinachoweza kumpunguza kasi ni kwamba sehemu kubwa ya utendaji inategemea zaidi mwitikio na ufanisi wa utumishi wa umma. Kama inavyohamika, utendaji wa sekta hiyo unahitaji mabadiliko ya jumla na siyo maboresho ya viraka.
Iwapo watumishi hao watafanya kazi kwa moyo na kuonyesha vipaji vyao bila ya woga wowote Serikali hii itafanikiwa zaidi na kuweka nafasi nzuri zaidi ya kurudi 2020. Ila, ikishindwa ndiyo utakuwa mwisho wake.
Nifuate kupitia Twitter @nuzulack





Monday, May 4, 2015

Wakati wa vijana kuacha mawazo ya kuajiriwa ni sasa


Ni kawaida kwa vijana wengi nchini kuwa na ndoto lukuki za mafanikio wanapoingia vyuo vikuu na vyuo vya kati. Asilimia kubwa huamini kozi wanazochagua na kusomea zitawapatia mafanikio ya haraka zaidi katika maisha.
Dhana hiyo huwafanya kuchagua kozi nzuri ambazo wakihitimu bila shaka watakua mameneja au watu wenye nafasi nzuri zaidi katika kampuni au mashirika makubwa ya umma.
Katika mawazo hayo ya ‘kusadikika’ huwa kuna mipango mingi ya kutekeleza mara baada ya kumaliza elimu zao ikiwamo kupata kazi haraka katika kampuni wanazotarajia kufanya, kuoa au kuolewa na wachache sana huwaza kuwekeza.
Hata hivyo mambo huwa ni magumu pale wanapomaliza stashahada au shahada zao kwa kukosa ajira ambazo huaribu mipango mingine yote. Kwa kiasi kikubwa ajira ndiyo msingi wa mipango mingi ya vijana hivyo ikikosekana kila kitu kinazama.
Nakumbuka hata mimi nilipata wakati mgumu kuchagua kozi ya kusoma kutokana na ushawishi mkubwa niliokuwa na upata kwa wakubwa zangu kuchagua masomo waliyoyaita ya ‘pesa pesa’.
Katika kundi la watu wote waliokuwa wakinishauri hakuna aliyeniambia kuwa nikienda kusoma Mlimani nitumie masomo hayo ili niweze kupata ufahamu wa kuwekeza.

Hakuna aliyethubutu kuniambia kuwa nikiwa shule nitunze fedha kidogo ntakazokuwa napata kwenye mkopo wa elimu ya juu au kutafuta ‘dili’ za muda mfupi zitakazoniongezea kipato kitakachosaidia kuanzisha biashara zangu.
Aina hiyo ya ushauri inazidi kuangamiza asilimia kubwa ya vijana nchini hasa wanaobahatika kupitia vyuo vikuu. Dhana ya kijamaa ya miaka 35 iliyopita ya kupata kazi baada ya chuo bado inatutafuna na kutufanya tuwe watumwa wa ajira.
Vijana wengi tumekuwa waoga wa kujaribu kujiajiri na kujikuta tunabaki mtaani hata baada ya kuhitimu kozi nzuri za biashara. Baadhi yetu hata kabla ya kujaribu kutafuta mawazo ya biashara tunakatishwa tamaa na nafsi zetu kuwa hatuwezi na hakuna vyanzo vya fedha kutuwezesha.
Hofu hiyo kama hiyo ndiyo anayoiita aliyekuwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Ludovick Utouh, kuwa ni matokeo ya kutobadilika ya mawazo ya muda mrefu ya kijamaa. Ni sehemu ya utegemezi wa kufikiri kila kitu kinafanywa na serikali na kuwapatia wananchi mambo mazuri.
Kizazi chetu kimebatika kuishi katika ulimwengu wa habari tele za biashara na uwekezaji lakini ni wachache sana wanaoweza wakatulia na kompyuta zao mpakato au simu wakasoma habari kama hizo.
Aina hiyo ya mawazo itaongeza idadi kubwa ya vijana wasio na ajira ambao baadhi ya wanasiasa wanaliita tatizo hilo kama bomu linalosubiri kulipuka. Iwapo kila mwaka wanahitimu zaidi ya 1 milioni na kuingia kwenye soko la ajira, na asilimia ndogo tu ndiyo wanaajiriwa kuna umuhimu mkubwa kujifunza kuwekeza.
Lakini mawazo na tabia ya kusubiri ajira yanaweza kuondolewa miongoni mwa vijana iwapo tunaweza kufanya yafuatayo;
Mosi, kujenga tabia ya kuwekeza kidogo kinachopatikana wakati tukiwa masomoni. Ni dhahiri kuna baadhi ya vijana wana matatizo ya kifedha lakini pia wapo wenye fedha kidogo zinazoweza kukusanywa taratibu benki pale wawapo masomoni zitakazowasaidia kupata mitaji watakapomaliza vyuo.
Ukikusanya Sh3 milioni kwa miaka mitatu itakayotokana na kuhifadhi kiasi kidogo cha pesa zako na kufanya vibarua bila shaka inaweza kusaidia kuanzisha biashara yoyote itakayosaidia kuishi mjini.
Pili, usomaji wa taarifa mbalimbali utasaidia vijana wengi kupata taarifa za namna ya kuanzisha biashara kutoka kwa watu mbalimbali wenye uzoefu. Binafsi nimejiunga na mtandao kibao inayotoa mafunzo ya ujasiriamali kama yes.com, Forbes, Vijanatz.com, Buni hub na mingine lukuki.
Kwenye vyanzo hivyo vya habari unaweza kupata taarifa nyingi zikiwemo namna ya kupata mitaji kwa kuanzisha mawazo mazuri ya biashara. Kuna wawekezaji lukuki wanatafuta vijana wabunifu watakaokuja na mawazo mazuri ya biashara yatakayoleta faida kubwa kwa mwekezaji na jamii.
Tatu, kuunda mtandao wa vijana wenye malengo ya kibiashara kunaweza kutuepusha na bomu. Vijana tunatakiwa tuwe na uhusiano wa karibu wa kibiashara kwa kuunda mtandao. Aina ya mtandao kama huo unaweza kusadia kuunda wazo, kuwakutanisha na taasisi za kimataifa na za ndani zinazotoa mitaji isiyo na riba kwa njia ya ushindani wa mawazo. Pia, kupitia kikundi ni rahisi kuomba miadi na wajasiriamali wakubwa ili kupatiwa mafunzo ya kutoka kibiashara. Katika soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) kuna wawekezaji lukuki wanaotafuta maeneo ya kuwekeza ila hawajapata mawazo  na kumpuni nzuri za chini na kati.
Mbinu kama hizo zinaweza kuwatoa vijana woga katika kufanya biashara na hatimaye kupunguza idadi ya wanaotegemea ajira. Kama asilimia kubwa ya vijana waliosoma watakuwa wanawaza ujasiriamali basi kuna kila dalili kuwa ajira nyingi zitatengenezwa na kupunguza kundi la wasio na ajira wenye elimu na ujuzi.



Sunday, April 12, 2015

Siasa zitaiangamiza Sumatra, sekta ya Uchukuzi

Moja ya vipindi vigumu kwa Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) mwaka huu ni hiki inapotakiwa kufanya aumuzi wa kutangaza nauli mpya za usafiri wa umma.
Kwa kipindi cha miezi sita sasa mamlaka hiyo imekuwa aking’ang’anizwa na wadau na viongozi serikalini ishushe nauli kutokana na kushuka kwa bei ya mafuta katika soko la dunia.
Pamoja na Sumatra kupinga mara kadhaa kuwa mabadiliko yasingefanyika haraka kwa sababu mafuta hushuka na kupaa kwa muda mfupi, wadau hao wakiwemo Baraza la Kutetea Watumiaji wa Uchukuzi (Sumatra CCC) walizidi kuongeza presha ya kushusha nauli.
Sumatra ilishasisitiza kuwa bei ya mafuta inachukua sehemu ndogo tu ya vigezo vya ukokotoaji nauli mpya na zipo gharama nyingine za uendeshaji kama vipuri, bima, mishahara, kodi na mengineyo.
Ni dhahiri kuwa kwa zaidi ya miezi sita wamiliki wa daladala na mabasi ya masafa marefu walipata faida zaidi baada ya kushuka kwa mafuta pasina nauli kushuka na wananchi nao walinyimwa unafuu wa nauli ambao ungesaidia kukuza shughuli zao za kiuchumi.
Tofauti na miaka iliyopita, katikati ya mwaka jana hadi Machi mwaka huu mafuta yalishuka sana kiasi cha Petroli kufikia Sh1,650 jijini Dar es Salaam, bei ambayo ilifikiwa miaka minne iliyopita.
Baada ya mashinikizo, Sumatra ilianza kukusanya maoni ya wadau kama sheria inavyowataka ili kupata mitazamo tofauti ya kutekeleza zoezi hilo.
Katika mkutano uliofanyika Dar es Salaam Machi 18, wamiliki daladala walipinga ushushaji nauli wakihofia mafuta yangepanda bei zaidi na wakatishia iwapo nauli itashushwa, wataanzsisha nauli kwa askari wa majeshi yote.
Wakati Sumatra ikiyafanyia kazi maoni na kufuatilia hali ya soko, Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta wiki iliyopita aliigiza tena mamlaka hiyo kuharakisha majadiriano na wadau na kisha kutangaza nauli mpya ndani ya juma hilo. Hata hivyo, mpaka sasa nauli mpya hazijatangazwa.
Presha kama hizo ni changamoto na kipimo cha uweledi na ufanisi kwa mamlaka za udhibiti nchini. Kuna kila dalili pia kuwa Sumatra inahofia kufanya uamuzi huo isionekane ya ‘kijinga’ na isiyofuata uweledi kutokana na hali halisi ya soko dhidi ya siasa.
Kama Wachumi wengi walivyoonya awali, bei ya mafuta imeanza kupanda tena hata kabla ya nauli mpya kutangazwa. Petroli mwezi huu, Dar es Salaam inauzwa Sh103 zaidi ya bei ya Machi ya Sh1652. Dizeli imepanda kwa Sh109 na Mafuta ya Taa kwa Sh132.
Shilingi nayo imezidi kuporomoka kutokana na kuongezeka thamani ya Dola ya Marekani ulimwenguni na sasa Dola moja inabadilishwa kwa Sh1, 850. Vipuri na mabasi huingizwa nchini na wafanyabiashara wake huathiriwa sana na udhaifu wa thamani ya Shilingi.
Hali ya kisiasa mwaka huu inayohusiana na Uchaguzi Mkuu inaweza kuathiri mwenendo wa kiuchumi kutokana na wawekezaji wengi kuhofia hatari za kiuwekezaji na mabadiliko ya kiutawala yanayoweza kutokea.
Pia, kuna kila dalili bei ya mafuta ikazidi kupanda. Takwimu za Benki ya Dunia (WB) zinaonyesha wastani wa bei ya mafuta ghafi katika soko la dunia kwa mwezi Februari iliongezeka hadi Dola za Marekani 54.93 (Sh101, 600) kwa pipa kutoka bei ya chini kuliko zote kwa miaka mitano ya Dola 47.45 (Sh87,780) kwa pipa mwezi Januari mwaka huu.
Ripoti ya Machi, 2015 ya nchi zinazozalisha mafuta sana ulimwenguni (Opec) inaonyesha mahitaji ya mafuta duniani mwaka huu yataongezeka kwa mapipa 1.17 milioni kwa siku na kufanya wastani wa mahitaji ya jumla kwa siku kuwa mapipa 92.37 milioni. Hii itapandisha bei ya nishati hiyo licha ya Marekani na Canada kwa kuzalisha mafuta mepesi mengi zaidi kwa bei ndogo.
Kwa mantiki hiyo na ukiachana na siasa, uamuzi wa Sumatra kushusha nauli ni mtego usiofanana hata kidogo na kipindi cha mabadiliko ya nauli mwaka 2009.
Iwapo Sumatra italazimishwa, itaingia kwenye mgogoro na wasafirishaji na kuwapa wananchi ahueni ya muda mfupi tu.
Mfumo mzuri na wa haraka wa ukokotoaji nauli uendao na soko ni kama unaotumika na Ewura kukotoa bei ya mafuta kila mwezi. Huo ungewaepusha Sumatra na kadhia na presha za kisiasa.
Sumatra ingekuwa inapitia nauli angalau kwa miezi sita au mwaka kuepusha unyonyaji kama ulitokea hivi karibuni kwa wananchi kwa kushindwa kushusha nauli haraka kwa mujibu wa mwenendo wa soko la mafuta.
Nuzulack Dausen ni mwandishi wa gazeti la Mwananchi anapatikana kupitia ndausen@tz.nationmedia.com au Twitter: @nuzulack






Thursday, February 12, 2015

Zawadi ya pekee kwa mke wangu mtarajiwa siku ya Valentine


Wasalaam kipenzi changu, mke wangu mtarajiwa.
Popote ulipo pokea salamu zangu hizi za dhati zisizo na tone la unafiki. Najua utakuwa umeshtuka kwanini nimekutumia barua hii leo, saa kadhaa kuelekea siku ya Wapendanao ambayo wazungu wanaiita Valentine. Usishtuke, nimekuletea zawadi yako maridhawa, kuwa mtulivu.
Tafadhari, usihudhunike kwa kuwa huna uhakika wa mpenzi au mume kwa sasa. Usisikitike na kujilaani kuwa una kasoro kwa kuwa wenzio wameshaanza pilikapilika za kuandaa au kupokea zawadi mahsusi za Valentine.
Inakuuma kutokuwa miongoni mwa hao thenashara lakini vumilia. Maisha sio maji ya mto yanayofuata mkondo wake. Maisha ni safari na waliombele ndiyo wanaowahi kufika bila kujali wamefika na kupata nini.
Bila shaka ulitegemea kupokea zawadi nzuri za maua mazuri ya waridi yaliyopulizwa manukato yenye rehe nzuri lakini kwa bahati mbaya ni haka kabarua ambako nimesahau kupulizia hata manukato ya ‘Nivea for Men’. Umakini wako kuisoma barua yangu kwa moyo ni zawadi tosha, zawadi nzuri kuliko hata Blackberry, Galaxy Note 4, Vits, IST au safari ya kutembelea visiwa vya Sanane na Zanzibar.
Najua masomo hayaendeki au kazi hazifanyiki huko uliko na unatamani siku ya Valentine iwe fupi, iishe na uachane na ‘mashida’ ya wenzio wanaoweka ‘status’ (ujumbe) mzuri na Selfie na wapenzi wao katika akaunti zao za Whatsapp, Instagram na Facebook.
Tuliza moyo na amini mimi nipo japo hatujawahi kuonana. Futa machozi na usiwaze kulazimisha penzi na mtu ambaye hakupendi, mimi nipo ila wasaa ulikuwa hauujafika wa kuanzisha uhusiano.
Naomba nisikuchoshe sana na maneno ya utangulizi yasiypunguza hata kidogo maumivu ya kovu la kuwa ‘single’ kwa sasa kwa sababu tu yule bepari mwenye gari uliyempenda alikuhadaa kuwa angekuoa lakini kumbe alikuwa na mke na watoto watatu. Au upo single kwa sababu tu vijana wanaoukuja bado hawajielewi au hawajaonyesa nia ya kukuoa na kukucheleweshea kamda kako ka kuolewa.

Thursday, December 4, 2014

KUTANA NA MUUZA MADAWA YA KULEVYA ALIYEKATWA MKONO, MGUU

 Nuzulack Dausen
UKIMUONA kwa mara ya kwanza ni vigumu kufikiri kama anaweza akawa amepitia katika mikasa migumu ya kutisha ya maisha kama ilivyomtokea.

Nguo zake kuukuu, nywele za chafu na ulemavu alionao vinaficha historia nzito aliyonayo katika maisha pamoja na utaalamu wa kuongea kwa ufasaha lugha za Kiingereza, Kiitaliano na Kireno licha ya kutosomea.
Huyu ndiye ‘Wa Mbele’ kijana aliyejiwekea ndoto za kuishi nje hasa Ulaya akiamini kuna maisha mazuri ambayo yangemfanya naye awe tajiri.
Hata hivyo ndoto zake hizo zilizimika pale hali hali ilivyobadilika na kujikuta akililia kurudi Tanzania baada ya kukumbana na mateso, manyanyaso, ukatili na biashara za kuhatarisha maisha kiasi cha kumfanya awe mlemavu wa viungo vya mwili uliomdhoofisha na kumharibia maisha yake.
Wa Mbele ambaye jina lake halisi ni Mbembele Said Lipwata nilikutana naye katika safari yangu Mjini Mtwara. Mbali na ulemavu wake  wa mguu na mkono wa kulia, bado ana uwezo mkubwa wa kutembea kwa kuruka kwa masafa marefu.
Anasema alizaliwa mwaka 1967 mkoani Mtwara, alikulia huko hadi mwaka 1976 alipojiunga na elimu ya msingi katika Shule ya Shangani.
“Hali duni ya maisha ilinifanya nimkimbie baba aliyekuwa akiishi Mtwara, kwenda kwa mama Magomeni Kagera Jijini Dar es salaam, niliendelea na masomo yangu huko” anasimulia Mbembele akieleza kuwa wazazi wake hawakuwa wakiishi pamoja.
Kaka zake wakubwa walikuwa wanajishughulisha na kazi za ubaharia jambo ambalo lilimpa matumiani makubwa ya kukamilisha ndoto ambazo alikuwa nazo kwa miaka mingi kwamba siku moja angezamia kwenda Ulaya akiamini angepata maisha mazuri.
Baada ya kumaliza masomo yake ya msingi mwaka 1983, Mbembele hakuwa na kazi ya kufanya kutokana na kushindwa kuendelea na masomo ya Sekondari, akaanza kuzunguka na kaka zake katika meli tofauti ndani ya Pwani ya Afrika Mashariki na kujaribu mbinu za kuzamia Ulaya.
Majaribio ya kuzamia
Kutokana na kupata uzoefu kidogo katika safari za meli, Mbembele anasema alianza majaribio ya kuzamia yeye na rafiki zake. Bandari ya Mtwara na Dar es salaam ndiyo vilikuwa vituo vikuu vya majaribio yao.

Wednesday, September 17, 2014

Mitandao ya kijamii isipoteze utu wetu na kudhalilisha waliokufa


Ndani ya mwezi mmoja watanzania tumeshuhudia mfulululizo wa ajali mbaya za mabasi ya masafa marefu zilizogharimu maisha ya watu zaidi ya 50 na kuwaacha wengine wakiwa majeruhi.
Tofauti na ajali zilizokuwa zikitokea miaka ya nyuma, ambazo waharifu walikuwa wakiiba mali za majeruhi na marehemu, safari hii kuna aina mpya ya uhalifu: uzalilishaji.
Mara tu baada ya ajali hizo kutokea baadhi ya watu aidha walionusurika au mashuhuda walijikuta wakiacha kusaidia majeruhi na kurekodi video au picha za kutisha na kuweka mtandaoni.
Asilimia kubwa ya picha hizo zimesambaa kwa kasi sana ndani ya majuma matatu haya na sasa zimekuwa zikipatikana kwa haraka bila hata kuangalia utu wa majeruhi au marehemu hao.
Dakika chache baada ya kugongana mabasi mawili ya Mwanza Coach na J4 Express hivi karibuni mkoani Mara, baadhi ya picha za maiti waliotolewa ndani ya magari hayo zilisambazwa zikionyesha wamelala chini bila hata ya kufunikwa.
 Sanjari na picha hizo, pia kulikuwapo na nyingine ilionyesha watu wawili wakiwa wananing’inia kwenye moja ya mabasi hayo baada ya sehemu za miili kunasa kwenye viti.
Picha hiyo ambayo inaonyesha maiti hao--wanaoweza kutambulika--wakiwa wamening’iniza vichwa vyao mtawalia huku damu nyingi zikichuruzika.
Pia, siku kadhaa baada ya ajali hiyo, ilitokea nyingine wilayani Kilosa ambayo iliua watu wanne na kujeruhi 35 baada ya basi walilokuwa wakisafiria kutoka dar es Salaam kwenda Tabora kuanguka eneo l la Berega.
Kama ilivyoa ada, watu hao ‘waandishi wa habari’ wa kisasa walisambaza tena picha za marehemu wanne wakiwa wamelazwa chini baada ya ajali.
Ndani ya saa 24 tena iklitokea ajali nyingine katika eneo la Tangi Bovu Jijini Dar es Salaam ambapo Lori lilipita basi na kuwagonga vibaya mwendesha pikipiki na abiria wake. 
Mwili wa dereva ulitupwa mtaroni wakati ule wa abiria ulichubuliwa na kugawanywa nusu baada ya kuburutwa na gari hilo.
Kama mchezo tena , picha za ajali hiyo zilisambazwa katika mitandao ya kijamii kama blogu, Whatsapp, facebook, Twitter na mingineyo. Pamoja, na uwingi wa mitandao hiyo, matumizi ya whatsapp ndiyo yamezidisha hali hiyo na inaonyesha jinsi gani Watanzania tulivyochanyikiwa na teknolojia ya mitandao ya kijamii.
Wengi tunaotumia mitandao hiyo hapana shaka tumeshatumiwa au tumeziona picha hizo tena zaidi hata ambazo nimezitumia kama mfano.
Katika ulimwengu wa dijitali ni dhahiri tunatakiwa kwenda na wakati hususan mabadiliko ya teknolojia. Hata sisi waandishi tunaofanyia katika vyombo vya habari vilivyo na sera zake na kuaminika kwa jamii tunapaswa kufanya hivyo lakini kwa kuzingatia maadili na utu wa watu.
Matumizi ya mitandao ya kijamii hayaepukiki katika kutoa habari za haraka lakini ni lazima tuheshimu utu wa Watanzania au yeyote yule ambayo anakutwa na maafa.
Usambazaji wa picha za kutisha na zinazozalilisha marehemu katika mitandao unatishia usalama wa taifa na unatia hofu kuwa Watanzania hawajali tena ndugu au rafiki zao.
Naamini wengi wanaopiga picha hizo hawajakutwa na majanga kama hayo kiasi cha mama, baba, kaka au wajomba zao kupatwa na ajali na miili yao kuwa miongoni ya ile inayoisambazwa katika mitandao.
Kuweka picha katika mitandao hiyo kunaziumiza kisaikolojia familia za ndugu waliopoteza maisha hasa zile zinazooneka wazi na katika hali isiyotakiwa kuoneshwa kwa mujibu wa mila zetu.
Pia, kunatia hasira kiasi cha kutengeneza kisasi iwapo ndugu hao wakibaini msambazaji na kuleta mambo ambayo taifa la umoja na upendo kama letu hatutaka tushuhudie.
Binafsi sipingani na uchukuaji wa picha za matukio hayo lakini uangalifu mkubwa unatakiwa kulinda heshima zetu na amani yetu kwa kusambaza picha ambazo haziogopeshi au kuzalilisha watu kama inavyoendelea nchini.
Nchi zilizoendelea, ambako teknolojia ya mitandao ya kijamii ilianzia, usambazaji wa picha kama hizo umepitwa na wakati na wameona haufai kwa ustawi wa taifa.
Mitandao ya kijamii kama hii itumike kutuunganisha sio kubomoa uhusiano wetu. Picha hisani ya socialmediamarketing.com
Wakati wa maafa kama hayo wenzetu hujumuika kwa pamoja na kutumia mitandao hiyo kukusanya michango ya fedha na damu kuchangia matibabu na kuokoa maisha ya majeruhi.
Mfano mzuri ni nchini Kenya. Baada ya Shambulio la duka la Westigate na magaidi wa Alshabab Septemba mwaka jana, Wakenya waliungana na kuchangia damu na mali hadi majeruhi walipopata nafuu; hakuna aliyeweka picha ya marehemu akikenua meno baada ya kuuawa…kwanini sisi tunadhalilishana!?
Ifike kipindi tuache ushamba wa mitandao na utumiaji wa kamera ovyo kuzalilisha marehemu na majeruhi. Yatupasa kuvivaa viatu vya watu na familia zao na namna wanavyoumia kwa picha hizo kusambaa ili kutokomeza tabia hiyo.
Makala haya yalichapishwa awali Jumanne, 16 katika gazeti la Mwananchi.

Wednesday, December 11, 2013

My thought: Why South Africans booed Jacob Zuma?

By Nuzulack Dausen
As the world continues to mourn the loss of the world icon Nelson Mandela, many things emerges as point of unity as well as disunity. The Tuesday boo by South Africans to their president Jacob Zuma during the Mandela memorial service in Johannesburg can confirm my fear.
Contrary to what ought to be, the majority attended in FNB Stadium to mourn the departed hero showed more love to the US president Barack Obama than their loved, majority voted president.  They cheered Obama more than his host.
Like many spectators in the world who watched the event through the live television coverage, I felt something went wrong in a big and historic event like that—which was attended by more than 100 global leaders.
What caused South Africans to boob their president? Perhaps the pledges by the speakers in the service to follow Mandela’s path--angered many by the facts that their government failed to copy Madiba.


While the Mandela’s death unites the world, South Africans seems not united to their government. The boo points out some few weaknesses of the Zuma’s government that do not reflect the real picture of the Mandela legacy. People have showed a public discontent with their government.
The rampant corruption and frequent violation of human rights reported in the country have at least disconnected Mandela’s government and that of Mr Zuma. Perhaps this could be a reason why majority booed Mr Zuma during his speech on Tuesday.
The allegations facing the head of state on using tax payers’ money to refurbish luxurious houses continue to triumatise South Africans especially when they remember Madiba.  A recent public prosecutor’s report revealed that he spent $20 million in state funds expanding his private home outside Durban, including setting up a large swimming pool. However the government officials have justified that the money was spent on security upgrades.



Mandela--in a straight language--was selfless; he respected human rights by pioneering equality, dignity, unity and love that’s why the world crying for his loss.
South Africans fears what will happen after the death of their father. They are worried on the way the government manage public resources.
Also, the extra-judicial killings of the mine workers in Marikana a year ago pose another question on Zuma’s administration. It neither suggests Mandela’s legacy nor propose a better leadership that South Africans would like to have.
The government is still struggling to convince the world that the massacre was not carried by police deliberately instead was a defensive mechanism against the angry mine workers. It is sad to lose 34 people whose lives cuts short by their guards just because were struggling for their rights.
Apart from that, the South African unemployment rate is higher as it suggests the presence of inequality between those who have and not. Currently the unemployment rate stands at 25.6% according to the country's national statistics service.
A section of  mourners attended the special memorial service for the late Nelson Mandela at FNB Stadiumon Tuesday. Many leaders who paid tribute to the fallen hero asked the world to follow the Madiba's path.  Photo: Courtesy of AP.
Such acts return events that Madiba was against with. They are simply a manifestation of torture, segregation and inequality that the country had suffered during the Apartheid era.
Currently, Pretoria government has tough job to retain the Mandela’s image: to end the ever growing corruption, cleaning all elements of Apartheid policy, and lowering inequality. This will puts the government in a pure democratic world that human beings would like to be.


Monday, December 9, 2013

Poverty keeps away majority from high-tech electronics in Kenya

By Nuzulack Dausen
Kenyans generally do not consider buying electronic gadgets as a luxurious affair unlike other techno savvy countries in the developed world.
Majority say an ever increasing competition between electronics manufacturers in releasing high-tech gadgets does not affect their consumption pattern. Instead they are looking at affordability and availability of the gadgets that will help them to access basic services and help to boost their lives.
They said their pockets allows buying cheap mobile phones and Radios that will help them to communicate and gets instant information. Among of the highly mentioned basic mobile phones services were: calling and sending short messages.
They said designs and brands were luxury matters that they could not prefer much as they struggle to win their daily bread.
For the past five years the electronics manufacturing industry have been going high-tech as companies tries to show off their technological capabilities. The short interval of releasing flagship brands within the same company has challenged some people who confused with the daily released designs.
For instance, before a company could take months or a year to release a new brand of an electronic gadget like a mobile phone, Hi-fi, radio or a television set. But now it just take three months to release new devices; Samsung is a good example for unveiling Samsung Galaxy S4 and S3 plus gear in a minimum period of six months.
They also say the insecurity of places where majority lives and the spread of fake gadgets in the streets were additional obstacles to buy the highly sophisticated devices for those who can afford.
 “For me it is illogical to buy the most expensive phone or a television while staying in Kibera (the largest slums in Kenya) even if I have money. The security of a particular place determines what type of electronic equipment one should buy,” said Julius Mtala, a university student in Nairobi.
He insisted that an increasing counterfeits on electronics in the country has also pushed many people not to consider brand factors when they shop the gadgets.  The malice he added reduces the original strength of the brands; the reason majority opts for cheapest Chinese phones.
Despite the absence of majority interests to the highly sophisticated electronics equipment like mobile phones, Kenya mobile subscription has increased to 30.4 million in September 2012 from 29.7 million of the three months before.
According to the Communication Commission of Kenya (CCK) mobile penetration stood at 77.2 per cent in September 2012.
Christopher Mwole an entrepreneur in Nairobi said the most considerable mobile phone’s features he wants is ability to call his client and send short messages. The best he added is to access mobile financial services like M-Pesa—a powerful Safaricom mobile financial service. Watch the video.
Even though some are running for the basic and most affordable electronics, John Maina an electronic repairer at 4ntech Communications in the city says some people have been seeking advice on kind of gadgets should buy. The most frequent asked questions he says are whether the devices are novelty and their ability to offer high quality mobile applications disregard to cost.
John Maina, an electronic repairer  in his mobile phone repair shop in Nairobi. Some electronics buyers   have been seeking advice on high-tech specifications which considered by lower income earners as expensive to buy.
He however acknowledges that the number of people who asks for specific details about the high-tech devices is relative low. Even customers who bring smartphones to get repaired he adds are very few comparing to one bringing conventional phones.