Tuesday, January 22, 2013

MGAO WA MAJI KUWAKUMBA BAADHI YA WAKAZI WA DAR NA PWANI


Nuzulack Dausen

BAADHI ya meneo ya Jiji la Dar es salaam na  Mkoa wa Pwani yanatarajiwa kukabiliwa na mgao wa maji unaotokana na  uhaba wa huduma hiyo uliyosababishwa na kushuka kwa kiwango cha uzalishaji wa maji baada ya kuharibika kwa mashine za kusukuma maji katika mtambo wa Ruvu Juu.

Hayo yamebainishwa na Shirika la Majisafi na Majitaka la Mkoa wa Dar es salaam( Dawasco) katika taarifa yake iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana  iliyolenga kuujulisha umma kukabiliana na tatizo hilo.

Taarifa hiyo ilisema maeneo yatakayoathirika ni Mlandizi, Visiga, Kongowe, Kibaha, Kwa Mathias, Picha ya Ndege, Maili Moja, Kiluvya, Kibamba, eneo lote la Mbezi, Golani, Kapinga, Mbuzi 40, King’ong’o, eneo lote la Kimara.

Maeneo mengine ni Changanyikeni, Ubungo Msewe, Ubungo Kibo, Ubungo Maji, Kilungule, Kibangu, Tanesco, Mandela Road, Mabibo  Hostel, makubuli, Matumbi, Tabata Bima, tabata Mawenzi, tabata Kimanga, tabata Kisiwani, Kisukuru, Tabata Chang’ambe na segerea.

“Matengenezo ya mashine hizo yanaendelea ili huduma ziweze kurudi katika mzunguko wake wa kawaida haraka iwezekanavyo” ilibainisha taarifa hiyo.


No comments:

Post a Comment