DAR ES SALAAM – Kampuni ya uchimbaji madini ya African
Barrick Gold (ABG) inafuraha kutoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko
wa Maendeleo wa ABG tangu kuanzishwa kwake mnamo Septemba 2011.
Mfuko huu umesimamia uwekezaji wa kampuni ya ABG kwenye
jamii katika kipindi kilichopita cha miezi 18 na kufanikiwa kutekeleza zaidi ya
miradi 50 yenye thamani ya dola za Marekani milioni 7.5 (takriban shilingi
bilioni 12 katika kipindi cha mwaka 2011/12.
Greg Hawkins, Afisa Mtendaji Mkuu wa ABG, amesema:
“Tunafurahi kuona mafanikio makubwa ambayo Mfuko wa Maendeleo wa ABG umeyapata
kwenye kipindi cha miezi 18 mpaka sasa. Tulianzisha Mfuko huu kama sehemu ya
jitihada zetu za kuchangia kwenye maendeleo endelevu nchini Tanzania na tayari
tumeona mafanikio makubwa kwenye zaidi ya miradi 50 mpaka sasa."
"Tunaendelea kuweka msisitizo kuhakikisha kuwa jamii
zinazotuzunguka zinapata faida kutokana na kuwepo wa shughuli zetu kwenye
maeneo yao na ninafurahi kutangaza kuwa kampuni ya ABG itaendelea kutenga dola
za Marekani milioni 10 kila mwaka kwa ajili ya uwekezaji wa Mfuko wa Maendeleo
wa ABG kwa mwaka 2013."
Mpaka hii leo, Mfuko wa Maendeleo wa ABG umewekeza dola
za Marekani milioni 2.2 (zaidi ya shilingi bilioni 3.6) kusaidia kuboresha afya
ya umma kwenye jamii zinazozunguko migodi yake.
Mfuko huu pia umesaidia kujenga miundombinu na
kuwawezesha wananchi wapate huduma za afya ya msingi na za hospitali ya rufaa.
Pia Mfuko umewekeza kuwapatia mafunzo wafanyakazi wa sekta ya afya ili waweze kuboresha
upatikanaji wa huduma za afya.
Kwa upande wa elimu, Mfuko umetumia zaidi za dola za
Marekani milioni 1.9 (takriban shilingi bilioni 3) kuwekeza kwenye sekta hii
muhimu. Uwekezaji wa Mfuko huu umesaidia kujenga shule mpya na kuongeza idadi
ya madarasa kwenye shule nyingine ili kuwapa watoto wengi zaidi fursa ya kupata
elimu bora.
Mfuko pia umewekeza kwenye ujenzi wa nyumba za walimu,
mabweni ya wanafunzi, na maabara ya masomo ya sayansi, sambamba na kuboresha
miundombinu mingine ya shule ili kuleta ufanisi kwenye utoaji wa huduma na
kuboresha mazingira ya elimu.
Mfuko wa Maendeleo wa ABG pia umewekeza dola za Marekani
milioni 1.4 (sawa na shilingi bilioni 2.2) kuhakikisha upatikanaji wa huduma za
maji safi ikiwa ni moja ya michango yake kwenye maendeleo ya jamii.
Kwenye mgodi wa North Mara uliopo wilaya ya Tarime, Mfuko
umewekeza dola za Marekani
800,000 (sawa na shilingi bilioni 1.3) kuchimba visima
vya maji ili kuwasaidia wananchi wapate maji safi na salama ya kunywa.
Ili kuboresha maisha ya wananchi kwenye jamii
zinazozunguka migodi yetu minne, Mfuko wa Maendeleo wa ABG umewekeza dola za
Marekani 1.4 milioni (zaidi ya shilingi bilioni 2) kwenye miradi mbalimbali ya
maendeleo ya jamii.
“Tumeanza kuona mafanikio kwenye uwekezaji wetu wa jamii na
tutandelea na njia hiyo. Uamuzi wa kuendelea kutenga dola za Marekani milioni
10 kwa Mfuko wa Maendeleo wa ABG mwaka
huu utawezesha tuendelee na kazi ambayo tumeianza, huku tukiweka msisitizo
zaidi kwenye maendeleo ya jamii,” amesema Hawkins.
Mfuko wa Maendeleo wa ABG unashirikiana na jamii husika
kubainisha vipaumbele vyao ili wanajamii wenyewe wawe mstari wa mbele kwenye
utekelezaji wa miradi. Kipaumbele kinatolewa kwa programu ambazo zinaendelezwa
kwa njia shirikishi huku kukiwa na ushirikiano wa karibu na washikadau
mbalimbali kutegemea na mahitaji ya jamii na mikakati ya maendeleo ya serikali.
Kampuni ya ABG inalipa gharama zote za uendeshaji wa
Mfuko wa Maendeleo wa ABG ili kuhakikisha kuwa asilimia 100 ya fedha za Mfuko
huo zinaenda moja kwa moja kwenye miradi ya jamii.
Kuhusu
Kampuni ya African Barrick Gold
ABG ni kampuni kubwa kuliko zote za uchimbaji wa dhahabu
Tanzania na ni kati ya kampuni tano kubwa zaidi za uchimbaji wa dhahabu barani
Afrika. Tuna migodi minne ya dhahabu nchini (Bulyanhulu, Buzwagi, North Mara na
Tulawaka), yote ikiwa kaskazini magharibi mwa Tanzania na tuna miradi kadhaa ya
utafutaji wa madini kwenye hatua mbalimbali za uendelezaji.
Tunafanya shughuli zetu kwa kuzingatia wajibu wetu kwa
watu, mazingira na jamii ambayo inatuzunguka kama vitu vya msingi vya
kutuwezesha tufikie malengo yetu.
ABG imesajiliwa kwenye Soko la Hisa la London (LSE) kwa
kutumia alama ya ABG. Mnamo tarehe 7 Desemba 2011, ABG pia ilianza kuuza hisa
zake kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).
Nector
Pendaeli Foya,
Meneja
wa Mawasiliano na Mahusiano
Simu: (+255 22) 216 4229,
Barua pepe: nfoya@africanbarrickgold.com
www.africanbarrickgold.com
No comments:
Post a Comment