Tuesday, March 26, 2013

ACB YAZINDUA HUDUMA YA MOBILE MONEY



Benki ya Akiba Commercial Bank(ACB) imezindua rasmi huduma za kifedha kupitia simu za mkononi zitakazo wawezesha wateja wa benki hiyo kutuma na kupokea pesa kupitia mitandao ya simu ya M-pesa, Airtel Money na Tigo pesa.

Akizindua huduma hiyo jijini Dar es salaam jana baada ya kutiliana saini ya ushirika na Kampuni ya Selcom Wireless, Mkurugenzi Mtendaji wa ACB John Lwande alisema wateja wa benki hiyo wataweza kutuma na kupokea pesa mahali popote walipo nchini bila kwenda kwenye tawi la benki.

“Mteja aliyejisajiri na Mobile money ya ACB anaweza kutuma pesa na kupokea kwa M-pesa kupitia akaunti yake ya simu inayoitwa Mobile Walet. Pia ataweza kutoa pesa kutoka kwenye akaunti ya ACB na kutuma kwenye akaunti za Airtel Money na Tigo pesa” alisema Lwande.

Mbali na huduma hizo za kutuma na kupkea pesa, wateja hao wateweza kurejesha mikopo benki bila kwenda kwenda kwenye tawi la benki na kupunguza gharama za muda na fedha.

Alizitaja faida za kujiunga na huduma hiyo kuwa ni urahisi wa kujiunga na kutumia huduma hizo za kifedha zinazopatikana nchi nzima, kutunza muda na pesa, na pia ni hatua muhimu za kimaendeleo za benki hiyo tangu ilipoanzishwa mwaka 1997.

“Wateja wa mitandao yote mitatu tunayoshirikiana nayo wataweza kutuma pesa hadi kiwango cha milioni 1 kwa gharama ya Sh1000 tu” alibanisha Lwande.


Alisema kuwa wateja hao pia wataweza kupata taarifa za salio la akaunti zao, taarifa fupi za kibenki pamoja na huduma za LUKU, Startimes, na DSTV.

“Wateja wasiwe na hofu kuhusu suala la usalama tumeshajipanga kuhakikisha hakuna tatizo katika muamala utakaofanyika kutoka benki kwenda katika mitandao hiyo na kuleta usumbufu na ikitokea hali hiyo tulishulikia haraka sana tatizo hilo” alisisitiza.
Mkurugenzi Mtendaji wa ACB John Lwande(katikati) akibadilishana mkataba na Mkurugenzi mtendaji wa Selcom Wireless Sammer Hirji(kulia) ma kushoto ni Meneja Mkuu wa idara ya ICT wa benki ya ACB.

No comments:

Post a Comment