Sunday, December 9, 2012

DK. BILAL AZINDUA DHL HOUSE

Na Nuzulack Dausen

Makamu wa Rais Dk Mohamed Gharib Bilal mwishoni mwa wiki iliyopita alizindua rasmi jengo  la kuhifadhia mizigo na ofisi za kampuni  ya DHL Express (DHL House)  lilopo ndani ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam ikiwa ni moja za jitahada za kampuni hiyo kurahisa na kuongeza ufanisi katika usafirishaji wa mizigo ya nje na ndani ya nchi.

Akizindua jengo hilo Dk Bilal alisema ujenzi wa jengo hilo unaonyesha wazi kuwa DHL imepania kuboresha huduma zake nchini kwa kusafirisha mizigo mingi na kuhudumia wafanyabiashara wengi zaidi kwa kwa wakati.
Alisema Serikali itaenedela kuboresha miundombinu ili kutengeneza mazingira rafiki kwa uwekezaji.

Aidha, Bilal aliwataka wawekezaji wote nchini kuiga mfano wa DHL wa kuajiri asilimia 99 ya wafanyakazi wazawa huku asilimia 40 kati yao wakiwa wanawake.

Alisema iwapo wawekezaji wataongeza imani kwa wazawa kwa kuwapa ajira basi tatizo la ajira linalolikumba taifa litatokemezwa na kuongeza kuwa wataalamu wazawa wapewe kipaumbele katika zabuni mbalimbali jambo litakalo ongeza tija kwa uchumi na maendeleo ya nchi.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa DHL nchini Braise De Souza alisema Kampuni yake itaendelea kuboresha huduma zake kwa kiwango cha juu na kuongeza kuwa wataendelea kuchangia masuala mbalimbali ya maendeleo ya kijamii kama kutunza mazingira, afya, elimu na kushughulikia masuala mbalimabali ya majanga ya dharura yanayolikumba taifa.

“Kazi yetu si usafirishaji pekee bali tunasghulikia pia na masuala ya kijamii kama kusaidia watoto hosptali ya Muhimbili, kutoa ajira kwa wanawake kwa asilimia nyingi zaidi, ma hivi karibuni tulidhamini tuzo ya Women of Determination iliyofanyika mwanzoni mwa mwezi huu” alibainisha De Douza.

Sherehe hizo za Ufunguzi pia zilihudhuriwa na Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe, Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar Suleiman Rashidi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Said meck Sadiq na wakurugenzi
Viongozi wa Idara mbalimbali za DHL Express wakiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa Serikali waliohudhuria uzinduzi wa jengo la kuhifadhia mizigo na ofisi la DHL Express House.

Mshindi wa tuzo za Women of Determination Award Nusra Mohamed akiwa na Viongozi waliohudhuria uzinduzi wa DHL Express.

Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal (kushoto) akifungua rasmi jengo la DHL Express mwishoni mwa wiki. katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa DHL Blaise De Souza na kulia ni Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe.

Mkurugenzi Mtendaji wa DHL Express( kushoto) akimpatia zawadi ya Kifaru Makamu wa Rais Dk Mohamed Bilal(katikati) na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa DSM Said Mecky Sadiq.

Dk Bilal akionyeshwa kitabu cha DHL EXpress na Mkurugenzi Mtendaji wa DHL Blaise De Souza.

No comments:

Post a Comment