Monday, December 3, 2012

JUAN MATA AKUBALI MADHAIFU YA CHELSEA


London, Uingereza.



MSHAMBUALIAJI wa mabingwa wa Ulaya (Chelsea) Juan Mata amesema kuwa kipigo kikali walichokipata kutoka kwa West Ham cha 3-1 mwishoni mwa wiki iliyopita kilitokana na kupoteza nafasi nyingi walizozipata hasa katika kipindi cha kwanza.


Mhispania huyo aliifungia timu yake bao la kuongoza katika kipindi cha kwanza kwa kumalizia pasi aliyoipata baada ya kazi nzuri ya Victor Moses na Fernando Torres ambapo bado nafasi nyingi za kufunga zilijitokeza bila kutumiwa.


Mshikanyundo Carlton Cole wa West Ham alipata bao baada ya saa moja na kufanya matokeo kuwa suluhu na baadaye wakaongeza bao mbili na kufanya Mabingwa hao kughalagazwa vibaya.


“Hali ilizidi kuwa mbaya sana kipindi cha pili, kipindi cha kwanza tulipata nafasi za kufunga. Tuliwafunga na tukaongoza kwa muda kipindi cha kwanza” alisema Mata.


Alisema kila mtua aliona kuwa  kipindi cha pili hawakucheza vizuri na kusababisha kupigwa bao tatu na Washikanyundo hao hali iliyosababisha kutoyarudisha mabao hayo kwa haraka.


Mata aliongeza kuwa toka ushindi wao wa mwisho wa Ligi dhidi ya Tottenham Hotspurs katika dimba la Whitepark Lane mwezi October wameambulia  pointi  4 tu dhidi ya 21 walizotakiwa wavune. 


“Inabidi tubadilike na kujiboresha, michezo huwa daima dakika 90 au 95. Tulitarajia  wangetumia nafasi za mipira mirefu ambayo wangepata na walifanya hivyo na kushinda bao la pili” alisema Mata.


Wiki chache za mwisho tumeshuhudia timu yetu ikishuka na kupoteza pointi muhimu, kuna haja ya kubadilika iwapo tunahitajji kushinda ubingwa wa ligi kuu msimu huu” aliongeza Mata.


Chelsea inazidi kuvurunda kwenye ligi na ligi ya Mabingwa  hasa baada ya kumfukuza kazi kocha aliyewapa mafanikio makubwa msimu uliyepita Roberto Di Matteo mwishoni mwa mwezi uliopita.


Imetayarishwa na Nuzulack Dausen kwa Msaada wa Mtandao.





No comments:

Post a Comment