Saturday, December 1, 2012

ANAOMBA MSAADA WA KUSOMESHWA



Nuzulack Dausen

MKAZI wa Tabata Kisukuru Jijini Dar es salaam Mahamoud Said (22) (pichani juu) anawaomba Wasamaria wema kokote nchini kumsaidia msaada wa fedha zitakazomsaidia kumalizia  gharama za masomo  yake.

Said ni mlemavu wa mkono asiyejiweza ambaye amefanikiwa kupata udahili wa masomo ngazi ya cheti katika Chuo cha Utumishi wa Umma Kilichopo Jijini Tanga lakini ameshindwa kujiunga mapema na Chuo hicho baada kukosa fedha.

Anasema kuwa alipata ulemavu wa mkono mwaka 1998 wakati akicheza mpira ambapo miaka miwili baadaye ulianza kutoa funza ndipo daktari aliamuru mkono huo kukatwa ili kumnusuru maisha yake.
Ombi hilo linakuja baada ya kupata msaada wa ada kutoka Shirika lisilo la Kiserikali la World Vision ambalo lilimsaidia kiasi cha Shilingi laki nane ambayo inatosheleza kulipia karo kwa mwaka mmoja tu. 

Kiwango hicho kilichobaki kinanajumuisha  fedha za kujikimu, nauli, sare, vifaa vya kusomea pamoja na michango yote ya Chuoni.

Awali habari ya kuomba msaada huo ziliandikwa kwenye gazeti la Mwananchi tarehe 27 Novemba mwaka huu kuhusu ombi la msaada wa kusomeshwa masomo hayo lakini kwa bahati mbaya hakuna aliyejitokeza kumsaidia, hata hivyo anawaomba wasamaria wema kujitolea ili aweze kufanikisha masomo yake.

Yeyote mwenye mapenzi mema na mwenye nia ya kumsaidia tafadhari apige simu au achangie  kupitia M-pesa namba 0766 469 548 au Tigo Pesa namba 0717 511 295.

No comments:

Post a Comment