Friday, August 12, 2011

BP bado ngangari mgomo wa mafuta


                             Moja ya vituo vya mafuta vya BP kikiwa hakitoi huduma ya
                                        mafuta hata baada ya masaa 24 ya serikali kupita.

       Baada ya Watanzania kukosa nishati ya mafuta kwa takriban siku tano mfulilizo baadhi ya vituo vilianza kutoa mafuta haraka mara tu baada ya Waziri mwenye dhamana ya nishati hiyo kutoa masaa 24 kwa wote wanaohusika na usambazi au uuzaji wa nishati hiyo. Hadi kufikia alhamisi ya tarehe 11 asilimia ya kubwa ya vituo hivyo vya mafuta vilianza kuuza nishati hiyo kwa wananchi waliokuwa wamechoshwa na uadimu wa nishati hiyo. Hata hivyo baadhi ya vituo vingine vya mafuta kama kampuni kongwe hapa nchini Brtiish Petroleum (BP) ambapo Serikali ya Tanzania ina hisa Asilimia hamsini havitoi huduma hiyo licha ya masaa 24 ya serikali kupita. 
      Wananchi wengi bado wana maswali  mengi vichwani mwao kuhusu ukaidi huu wa BP na makampuni mengine hasa ambayo hayana majina kwa kutokutii amri ya serikali. Naamini kuwa na hivyo ndivyo inavyotakiwa kuwa kwamba hakuna kitu kingime zaidi ya Serikali. Serikali ndio kila kitu katika masuala ya huduma kwa wananchi. Uwepo wa makampuni binafsi ni moja ya njia tu za kuongeza ufanisi na umakini katika utoaji huduma hitajika kwa Watanzania. Bado wananchi wengi hawana taarifa rasmi za kwanini BP haifanyi kazi? Hatutakiwi kulaumu  harakaharaka kuhusu hili suala bila ya uchunguzi na tafakari ya kina. Inawezekana kuwa jamaa ndio wameacha kabisa kuuza nishati hiyo au bado ipo njiani kuletwa nchini tayari kwa huduma. Hata kama majibu ndo hayo sisi kama wateja wa BP ilibidi tujulishwe hata kwa  njia ya magazeti na matangazo mengine Radioni na Televisheni kuwa huduma hii imesitishwa kwa muda na waombe radhi kwetu sisi wanachi ambao ni wateja wao. Iwapo watafanya hivyo watakuwa wamefuta kashfa ya kuwa wameigomea Serikali na kama sababu si hizo Serikali ichukue hatua kali dhidi ya kampuni hili hata kama wamegawana hisa.
        Ni matarajio yangu kuwa miaka na siku zijazo hatuoni tena uzembe na hasara zilizojitokeza kuhusiana  na mgomo wa wafanyabiashara wowote licha ya hawa wauza mafuta. Ni dharau kubwa kwa Serikali kusumbuliwa na wafanyabiashara. Na iwapo itatokea tena hivyo lazima tukubaliane kuwa Serikali yetu ni lobbied na wafanyabiashara na Sera zote zilizopo zinasadifu matakwa ya vigogo na wafanyabiashara na si wananchi. Hivyo basi Watanzania wote tuungane tena mara nyingine na siku nyingine litakapo tokea hili kuupinga mgomo na hata Serikali itakayokuwepo madarakani. Hatutakubali kuingizwa kwenye hasara za kizembe za nchi zima kwa Mabepari wawili.
       Mungu Ibariki Tanzania, Mungu tubariki watoto wa Tanzania!
    

No comments:

Post a Comment