Monday, August 1, 2011

"Nuru mpya ya mabadiliko hii hapa..."

Wapendwa Watanzania, yapata miaka 50 sasa tangu nchi yetu pendwa ilipopata uhuru toka kwa Mkoloni wa Kiingereza. Serikali nne tofauti zimetuongoza mpaka tumefika hapa tulipo toka ile ya Hayati Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius K. Nyerere, Mzee A.H. Mwinyi, Benjamin W. Mkapa na hii ya sasa ya Mheshimiwa Rais Jakaya M. Kikwete. Kama Mataifa mengine duniani yaliojikomboa kutoka kwa Mkoloni nchi yetu chini ya serikali zake imefanya mipango(Nation Building Projects) mbalimbali ili kuleta maendeleo kwa wananchi wake. Lakini licha ya michakato hiyo ya maendeleo bado Watanzania hatujapata matunda halisi ya Uhuru. Maisha magumu ndio Wimbo wetu kila siku.
      Hivyo basi ili kujenga mustakabali chanya kwa Watanzania wote nchini na nje ya nchi, mimi kama Mtanzania mpenda mabadiliko na ninaeguswa na harakati mabalimbali za watu binafsi na Taasisi mbalimbali katika kuleta maendeleo na kupigania haki mwiongoni mwetu (Watanzania) napenda kutumia blog hii kujadili mambo mabalimbali ya Kiuchumi, Kisiasa, Kijamii, Mazingira, Michezo na Burudani na mengine yanayotuhusu ili kujenga Tanzania yetu. Naahidi kushirikiana na kuyaendeleza mambo mazuri ya wote waliotangulia katika harakati hizi za kuijenga Tanzania bora na endelevu.
    Ewe Mtanzania!  ungana nami katika  nuru hii ya mabadiliko ya kweli kutoka leo  ili tuijenge Tanzania yetu.
    Mungu Ibariki Tanzania, Mungu tubariki Watoto wa Tanzania!

No comments:

Post a Comment