Wednesday, August 24, 2011

Langa: Madawa ya kulevya sasa basi!

       Msanii wa mziki wa Hiphop nchini Langa ameuthibitishia umma kuwa hatatumia tena Madawa ya kulevya kama zamani. Langa alibainisha hayo katika mahojiano na kipindi cha kupambana na madawa ya kulevya kilichorushwa hewani na Redio One chini ya Mtangazaji Abdallah Mwaipaya maarufu kama ABD majira ya Saa kumi na moja jioni siku ya Jumatano ya tarehe 24 mwezi huu.
       Langa alishiriki kipindi hicho pamoja na Bwana Jamal Mtisi wa Tume ya kupambana na kudhibiti Madawa ya kulevya na Mama Fatma Supa Tume ya kupambana na Madawa ya kulevy a Zanzibar. Katika maelezo yake Langa alikiri uwepo wa wasanii wanaotumia madawa ya kulevya kama ilivyokuwa kwake.
    Anasema baada ya kutumia kwa muda sasa madawa hayo kaona hayana faida kabisa na yanasababisha masuala mengine ya kibiashara na kimaisha kuzorota. Langa anafichua kuwa moja ya vitu vilivyochangia kazi zake za mziki kutokuwa sawa ni Madawa ya kulevya.
      Ili vijana wafanikiwe kimaisha hawana budi kuachana kabisa na madawa hayo hatari ambayo huleta uteja pamoja na kurukwa na akili. Langa alisema yupo radhi kuisaidia serikali katika jitahada za kupambana na Madawa ya kulevya kwa kutoa elimu kwa vijana wenzike na umma kwa ujumla. Ili kufanikisha anatoa elimu ya kutosha kuhusu madawa ya kulevya Langa aliwaomba wadau mbalimbali wa mambo haya pamoja na Serikali  kumfadhiri aweze kuanzisha NGO ya kupiga vita madawa ya kulevya.
     Ili kuonyesha kuwa  kashaachana na madawa ya kulevya na yupo kwenye mchakato wa kutoa elimu kwa jamii Langa katunga singo maalumu ya kuelimisha ambayo aliimba kwa akapera studioni hapo. Aliendelea kubainisha kuwa atarudi kwenye game kama zamani alipokuwa na kundi la mziki la Wakilisha lilokuwa likiundwa na yeye (Langa) , Witness na Shaa. Kwa mashabiki mnaombwa kukaa mkao wa kula kusikia vitu vipya vya msanii huyu ambaye kwa sasa anatamba kwa singo yake Pesapesa mkubwa wa kushawishi jamii nzima.
     Big up sana mzee Langa tunakutakia maisha mapya ya kimziki na masuala mengine ya maendeleo. endeleza juhudi hizo mpaka tupate uhuru mwingine kutoka kwenye madawa ya kulevya.

No comments:

Post a Comment