Monday, August 15, 2011

Huu ni mchezo mchafu ......

       Siku 12 baada ya serikali kutangaza kushushwa kwa bei ya mafuta nchini hali imerudi kama awali. EWURA imetangaza kuongezeka kwa bei ya mafuta ya Dizeli, Petrol na mafuta ya taa. Hadi kufikia leo asubuhi vituo vingi vya mafuta hapa jijini Dar es salaam na ngineko vilikuwa vimeshabadirisha bei na kutumia mpya zilizotangazwa na chombo hicho cha serikali. Ikumbukwe kwamba huu ni mwendelezo wa machungu kwa Watanzania wa kipato cha chini ambao walitarajia kuwa kushuka kwa bei ya mafuta kama ilivyotangazwa hapo agosti 3 kungewasaidia japo palikuwepo na usumbufu mkubwa wa upatikanaji wa mafuta wiki iliyopita.
    Hii nia hatua nyingine ambapo serikali itapata changamoto kutoka kwa wadau mbalimbali wa kupigania haki na maendeleo nchini. Kwangu mimi naweza nikasema huu ni mchezo mchafu "Siasa". Hapa naomba tuelewane kidogo ndugu wananchi wenzangu. Bei hii ya mafuta imepandishwa kukiwa na matukio makubwa ya kuihusianisha. Mosi ni kupitishwa kwa bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mapema juzi Jumamosi. Kabla hata masaa 24 ya kupitishwa kwa bajeti hiyo ewura wakapandisha mafuta. Hii inaweza ikatusaidia kufikiria mrorongo huu wa matatizo ya mafuta kama matimizo ya matakwa ya siasa na si kwa mahitaji ya wananchi. Pili, bei hii mpya ya mafuta imepanda wakati serikali ikiwa na mazungumzo ya kina na wafanyabiashara wa mafuta nchini na huku wengine wakiwa wamechukuliwa hatua madhubuti kama kampuni ya British Petrolium (BP). Kwa haraka naweza nikasema serikali imekuwa lobbied na wafanyabiashara hawa wa mafuta.
     Tukumbuke kuwa wakati Serikali inatangaza kushuka kwa bei ya nishati hii muhimu mnamo agosti 3 mwaka huu hali ya uchumi Duniani ilishaanza kuwa tete. Kwa hiyo tumepigwa changa la macho hapa. Ishu si kuanguka kwa thamani ya shilingi  yetu ila kuna sababu nyingine zaidi ya hiyo.
  Ewe Mtanzania tafakari!

1 comment:

  1. imeshakuwa tabia ya hii serikali kufanya vitu vya kulainisha wananchi bila ya kuangalia athari zake.
    sasa hii ya sasa n balaaaaa!

    ReplyDelete