Tuesday, August 23, 2011

Video ya Tajiri wa mahaba ya Cassim Mganga ni nomaaa!

     Tasnia ya mziki wa kizazi kipya inazidi kupanda chati kila uchwao. Wasanii wapya wanaongezeka huku wale wazamani nao wakiokoa status zao kuzuia kupotea katika game. Katika safari hiyo ya mabadiliko katika game wasanii wengi wakongwe wamepotea na kuacha idadi ndogo sana tofauti na ile ya wanaongezeka kila siku. Licha ya maendeleo hayo ya game la Bongo fleva kuna wasanii ambao wamekuwa wakifanya kazi zao vizuri na kufanya zipate sifa mbalimbali katika ulimwengu wa mziki huu wa kizazi kipya mmoja ya wasanii hao ni Cassim Mganga wa kundi la mziki la TIPTOP lenye maskani yake pale Manzese Jijini Dar es salaam.
Moja ya kipande cha video ya tajiri wa Mahaba

Sehemu nyingine ya video hiyo ikimuonyesha Cassim na mrembo wake kwenye video ya tajiri wa mahaba
    Tofauti na wasanii wanaotamba katika chati kwa sasa Cassim yeye anao wimbo wa tajiri wa Mahaba wenye asili ya Kitanzania. Wadau mbalimbali wa mziki huu wametokea kuukubali sana wimbo huu. "Ukiusikiliza kwa makini sana wimbo huu utagundua upo tofauti kidogo na hizi nyingine zinatamba kwenye Top ten mbalimbali za redio zetu, tofauti inakuja kwenye beat na style aliotumia mkali huyu wa nyimbo za malavidavi" anasema Feruuz mkazi wa Tabata Segerea. Nae Esther wa mitaa hiyohiyo ya Segerea alitoa mtazamo wake kuhusu wimbo huu akasema "Unajua bro tuache unafiki na wivu wa kijinga, wimbo wa tajiri wa mahaba wa Cassim ndo unaenikuna sana ila utamu unazidi sana nikiiona video yake kwenye TV steshen mbalimbali kila siku" alibainisha.
      Hata hivyo safari ya kujua ni video ipi msimu huu wa kusherekea miaka hamsini ya Uhuru inasadifu Utanzania wetu ilizidi kusonga mbele na kuuliza wadau mbalimbali wa mziki huu wakiwemo wauza CD, kanda na wasikilizaji. Lakini majibu yote yalisifia video ya wimbo huo wenye mahadhi ya kipwani.
    "Kweli Cassim ni nomaa hata video yake ipo You Tube inaquality zote. Nakupa big up sana kijana kaza buti na endelea kutoa vitu adimu kama hivyo kila siku ili kukuza game. keep it up!" anasifia muuza kanda mmoja wa Kariakoo.
    Sasa ni kazi yako Mtanzania kununua kazi za Cassim na si kudownload kama tulivyozoea, tujitahidi kusupport wasanii wetu ili watoe kazi nzuri zaidi kama hii. Tafadhari usiombe zikupite kazi hizi adimu. 
         Just Watch out today its more than good!

No comments:

Post a Comment