Monday, July 2, 2012


Happy Birthday!


Umetimia mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa blog hii, ilikua ni july 2011 na sasa ni july 2012. Yapo malengo mengi ambayo hayajatimizwa kama ilivyopangwa hapo awali. Lakini huo si mwisho wa kuifanya Blog hii kuwa bora zaidi na yenye chambuzi na habari za kina.

Ni dhahiri kwamba kushindwa kufikia malengo kwa asilimia mia ni moja ya dalili za kushindwa kutimiza mipango. Hata hivyo kushidwa kutimiza lengo ni changamoto kwangu, kunanipa nguvu ya kujipanga zaidi na kuandaa mipango ya muda mfupi  na mrefu ili kutimiza lengo.


Napenda kuwashukuru wasomaji na wachangiaji wote kwa kushiriki katika Blog hii. Pia shukrani za dhati ziwaendee wote ambao kwa namna moja au nyingine wamesaidia kuwapo kwa blog hii. Napenda tuungane wote kutimiza malengo kwa kuchangia habari na maoni mbalimbali ambayo yatakua chachu ya maendeleo ya jamii yetu ya Tanzania. 


Napenda niahidi kuwa sasa Blog hii itakuwa na taarifa za wakati kwa kushirikiana na viunganishi vingine vya chambuzi na habari. Hii ni moja ya njia ya kuzikusanya habari na chambuzi mbalimbali sehemu moja. Hii itasaidia kujifunza mengi kwa wakati. Tafadhari tusichoke kufuatilia Blog hii katika masuala yote ya siasa, uchumi, jamii, elimu, Sayansi na teknolojia na burudani.

Karibuni sana na msikose kuisoma Blog hii kila siku.
 Nuzulack J. Dausen

No comments:

Post a Comment